Zinazobamba

RC MAKONDA SASA AWAGEUKIA WAKAZI WA DARESALAAM



MWANDISHI WETU, DARESALAAM
 
MKUU wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amewataka wakazi wa Jiji hilo kuwa tayari kubadilika

Akizungumza na katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya maji Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda amesema, katika kuadhimisha Wiki maji, Mkoa wa Dar es Salaam umelenga kuwahamasisha na kuwaelimisha Wananchi, Viongozi wa Serikali za Mitaa pamoja na Kamati za Maji kuhusu namna bora ya usimamizi wa shughuli za maji katika maeneo yao ikiwemo na tarataibu za umiliki wa visima.
Aidha amesema kuwa  miradi ya visima vya dharura katika maeneo yasiyo na maji ya bomba ambapo ameeleza kuwa, DAWASA ina idadi ya visima 147, Manispaa za mkoa zina visima 789 na Taasisi na Watu binafsi visima 600.
Kwa upande wake Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) Bw. Kiula Kingu amesema kuwa, DAWASCO pamoja na DAWASA wamefanikiwa kuzuia upotevu wa maji kwa kiasi kikubwa ambapo kwa mwaka jana ulikuwa  ni asilimia 47 na mwaka huu umepungua na kufikia asilimia 38.6.
Naye Meneja Mahusiano ya Jamii Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Bi. Neli Msuya ameeleza kuwa, maeneo yote ya Dar es Salaam yasiyo na mtandao wa maji yamekuwa yakitengenezewa ramani (design) ili yawekewe mitandao hiyo ya maji ili maji yaweze kupatikana kwa wakazi wa maeneo hayo.
 
  Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni “Majisafi na Majitaka-Punguza Uchafuzi yatumike kwa Ufanisi (Water and Waste Water-Reduce and Reuse).