MEYA UKAWA ILALA AZIDI WABORESHEA WANANCHI WAKE,AZINDUA DARAJA MUHIMU,SOMA HAPO KUJUA
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko,
akikiwa amekata utepe ikiwa ni ishara ya kufungua rasmi daraja
linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya
Ilala, jijini Dar es salaam.
Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonesti (Chadema) akihutubia wakati wa ufunguzi wa daraja hilo
MSTAHIKI MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko
jana alifungua rasmi daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya
Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam.
Awali akizungumza katika hafla hiyo Mhandisi wa Manispaa ya Ilala ndugu
Benjamin Maziku alisema daraja hili limejengwa kwa takribani mwaka
mmoja na kugharimu Tsh.million 478 hadi kukamilika kwake leo hii.
Ujenzi wa daraja hili umesua sua kwa siku nyingi kutokana na sababu
mbali mbali lakini kutokana na usimamizi imara wa Mstahiki Meya wa Ilala
Mhe. Charles Kuyeko sasa historia imebadilika.
Meya Kuyeko akizungumza na umati wa wananchi waliokusanyika kushuhudia
ufunguzi huo amewasitiza kulilinda na kulitunza vyema daraja hilo kwani
limejengwa kwa kodi zao.
Awali, Meya akitoa historia ya daraja hilo amesema kuwa, waliokuwa
wanatakiwa kujenga daraja hilo ni wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad)
lakini kutokana na kusuasua kwao, Mimi (Meya) niamua kuingilia kati kwa
Manispaa kutenga Fedha kujenga daraja la muda ili kuwasaidia wananchi
wa Bonyokwa kuondokana na atha ya kuwa Kisiwa hususani wakati wa Mvua.