Zinazobamba

MAPYAA YAIBUKA SAKATA LA KAFULILA KUZUILIWA CLOUDS TV,SOMA HAPO KUJUA



http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2016/05/kafulila.jpg

NA KAROLI VINSENT
WAKATI aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini,David kafulila leo akizuiliwa kuongea moja kwa moja kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na kituo cha Luninga cha Clauds Tv kwa kile kilichoelezwa matatizo ya ufundi ndani  ya TV hiyo,

Sasa Mpya yameenza kuibuka juu ya sakata hilo baada ya kudaiwa kuwa Kiongozi wa juu aliyoko ndani ya utawala wa Rais John Magufuli ndio amehusika katika kutoa katazo wa kipindi hiko kurushwa hewani.(Fullhabari.blog limedokezwa)


Kafulila ambaye alikuwa mbunge wa NCCR mageuzi leo alikuwa amealikwa ndani ya Clouds Tv kwa sasa ili kuchambua masuala mbali mbali yanayohusu hali ya nchi katika kipindi cha 360 kilichotakiwa kuruka hewani majira ya saa mbili na nusu asubuhi.

Kwa Mujibu wa Mbunge huyo ambaye alisifika kwenye utawala wa awamu ya nne katika kupambana na kuibua kashfa ya Escrow ambayo iliitikisa serikali ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na kupelekea mawaziri kadhaa kujiuzulu,

 Ambapo amedai alifika kwenye studio na za Kituo hicho zilizopo Mikocheni Jijini dar es Salaam huku maandalizi mbali mbali ya kipindi hicho kuruka yalikuwa yamekamilika.
 
Ameleza maandalizi hayo ni kwa watangazaji wa kipindi hicho kuanza kutangaza pamoja na wapiga picha kuwa teyari ila gafla ikatokea   taarifa kuwa wakubwa wamekizuia kiipindi hicho bila ya kutaja sababu.

 Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wa kuaminika kutoka ndani ya Kituo hicho ambaye akutaka jina litajwe Mtandaoni ameuambia mtandao wa Fulhabari.blogs kuwa shinikizo la kipindi hicho lilitoka kwa mmoja wa vigogo walioko ndani ya serikali.

 “Kaka sikufichi,kwani leo Kafulila alitakiwa kuzungumza kwenye kipindi chetu ila tulikuwa tumeshajiandaa kabisa kwa ajili ya kipindi kuruka hewani, kama unavyojua kipindi kile ni cha moja kwa moja,tukapigiwa simu na watu wa juu serikalini tukaambiwa tuache kabisa kurusha kipindi hicho,sasa wewe unategemea tufanyaje kumbuka na sisi tuna watoto wanahitaji kwenye chooni”Kimesema Chanzo hicho.
Ameongeza kusema kuwa kwa sasa wanafanya kazi kwa uoga mkubwa jambo analodai kama hali ikienda hivyo basi wabunge wa upinzani na wanaharakati itakuwa vigumu kuitwa kwenye mijadala ya Runinga kwa kuhofia kufungiwa kwa Vituo vyao,
“Sahivi ndugu tunafanya kazi kwa hofu kubwa sana ,wewe mwenyewe umeona Redio Five kilichowakuta walimuhoji Mbunge Lema sahivi hawako hewani,hata kituo cha Itv walimuohi Mbunge Msigwa wakaishia kupigwa Faini ya mamilioni ye fedha na TCRA,sasa wewe unategemea nini ,sahivi hata sisi tumeanza kuingiwa na uoga kuwaita wapinzani”ameendelea kuongeza mtoa taarifa huyo.