Zinazobamba

MANISPAA YA ILALA YAFAFANUA KUHUSU TAARIFA YA UKATILI KWA WATOTO,SOMA HAPO KUJUA




 NA KAROLI VINSENT
MANISPAA ya Ilala imesema katika kipindi cha mwezi Januari hadi Agost mwaka huu jumla ya watoto 302 wameripotiwa kufanyiwa ukatili wa kingono.

Ambapo kati yao, watoto 130 ni wakike ambapo ni sawa na asilimia 43% wameripotiwa kubakawa,huku watoto wakiume 24 sawa na asilimia 7.9% wameripotiwa kufanyiwa vitendo vya kulawitiwa.

Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Afisa Uhusiano wa Manispaa hiyo,Tabu Shaibu wakati wa mkutano na waandishi wa habari ili kutoa ufafanuzi juu ya manispaa ya ilala kutajwa kuwa kinara kwa vitendo vya ubakaji.


Amesema kamati  ya ulinzi na usalama wa mtoto imefanya utafiti kupitia madawati mbali mbali ya kijinsia yaliyopo kwenye vituo vya Polisi katika manispaa hiyo wamebaini kuwepo kwa matukio hayo ya kinyama kwa watoto.

“Katika Tathimini ya awali iliofanywa imeonyesha kuwepo kwa vitendo  vya ukatili dhidi ya watoto hususani matukio ya ukatili wa kingono(watoto kubakwa na kulawitiwa) majumbani  kwa watoto chini ya miaka 18”amesema Afisa Shaibu.

Amesema Sababu waliyoibaini kupelekea kwa vitendo hivyo katika manispaahiyo imechangiwa na uwezo mdogo wa kujitetea kwa watoto hao jambo linalopelekea kufanyiwa vitendo hivyo,

Afisa huyo pia ametolea ufafanuzi ulioripotiwa na Vyombo vya habari kuwa kati ya watoto 10 katika manispaa ya ilala watoto 7 wamefanyiwa ukatili wa kingono,huku akidai ripoti hiyo haikuwa  sahihi.

Pamoja na hayo,Afisa Shaibu ametoa hofu wazazi na walezi wa watoto katika manispaa hiyo kuondoa hofu waliokuwa nayo kutokana na taarifa hiyo kwa watoto,