Zinazobamba

SHEIKH PONDA TENA,SAKATA LAKE KUFUKILIWA UPYAA,SOMA HAPO KUJUA




Sheikh Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania

SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini, bado anawindwa na mawakili wa serikali, anaandika Faki Sosi.

Mawakili hao wanapinga hukumu yake iliyotolewa na Richard Kabate, Hakimu Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro mwaka jana ya kumfutia makosa ikiwemo la uchochezi.

Jana katika Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Jaji, Edson Mkasimongwa, Bernard Kongola ambaye ni Wakili Mkuu Mwandamizi wa Serikali amesema kuwa, Jamhuri inapinga hukumu hiyo.

Mwaka 2013 Sheikh Ponda alishitakiwa kwa makosa matatu; la kwanza alidaiwa kuwaambia waumini wa Dini ya Kiislam kwamba, wasikubaliane na uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti zilizoanzishwa na Baraza Kuu la Waislam Tanzania kwa madai ni vibaraka wa CCM na serikali.

Shitaka la pili lilihusu kuwa, Sheikh Ponda aliwaambia Waislamu kwamba serikali ilipeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi ili kuwaua, kuwabaka na kuwatesa wananchi, kwa sababu asilimia 90 ya wakazi hao ni Waislamu.

Shitaka la tatu alidaiwa kulitendwa tarehe 10 Agosti mwaka 2013 kuwa, kauli yake katika shitaka la pili inadaiwa kuumiza imani za watu wengine kinyume cha kifungu cha sheria namba 390 na kanuni ya adhabu namba 35 cha mwaka 2002.

Wakili Kongola amesema, uamuzi uliotolewa na Hakimu Kabate haukuzingatia uzito wa ushahidi wa Kielekroniki uliofikishwa mbele ya mahakama yake.
Wakili Kongola amesema kuwa, hakimu alikosea aliposema kuwa hati ya mashitakaa ina upungufu kisheria  na kuwa Shekh Ponda hakuwa na nia ya kuwashawishi waumini kufanya kosa.
Amesema kuwa, hakimu alikosea pale aliposema  upande wa mashitka  haukuthibitisha mashitaka mahakamani. Rufaa hiyo imepangwa kuanza kusilizwa rasmi tarehe 30 Juni mwaka huu.
Mwishoni mwa Novemba mwaka jana, Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ilimuachia huru Sheikh Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama hiyo kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka.
Awali Bernard Kongola, Mwanasheria Kiongozi  wa Serikali  mbele ya Richard Kabate, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro alidai  kuwa, tarehe10 Agosti mwaka 2013, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Morogoro, Sheikh Ponda alifanya uchochezi jambo lililosababisha kufunguliwa mashitaka hayo matatu.
Na kwamba, awali katika agizo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyotolewa na Hakimu Victoria Nongwa tarehe 9 Mei mwaka 2010, Sheikh Ponda ndani ya mwaka mzima alitakiwa kuhubiri amani na kuwa raia mwema jambo ambalo alishindwa kulitekeleza.
Katika kesi yake Sheikh Ponda alikuwa akitetewa na wakili wake Juma Nassor

Hakuna maoni