Zinazobamba

WAZIRI MPANGO AKABIDHI OFISI TRA,ASEMA YEYE HATA KUWA WAZIRI WA KUOMBA OMBA KWA WAHISANI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Waziri wa Fedha na Mipango,Dkt Philip Mpango

WAZIRI wa Fedha na Mipango Dkt Philip Mpango amesema kamwe hata kuwa Waziri ambaye atakuwa omba omba na kuwategemea nchi wahisani.Anaandika KAROLI VINSENT     endelea nayo.
Hata hivyo,amesema kwa sasa wizara yake kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) watahakikisha wanawawekea mazingira mazuri wafanyabiashara wakubwa katika kulipa kodi.
      Waziri Mpango ameyasema hayo leo Jijini wakati alipokuwa akikabidhi ofisi aliyokuwa akihudumu nafasi ya ukaimu Kamishna mkuu wa TRA nchini kwa Kamishna mpya wa mamlaka hiyo,Alphayo Kidata ambaye awali alikuwa Katibu mkuu Wizara ya Ardhi,nyumba na Maendeleo na Makazi,
    Ambapo Waziri Mpango amesema nia ya serikali ya awamu ya tanu ni kuhakikisha inakusanya mapato yake ya ndani kwa kiasi kikubwa na kuondokana na kasumba ya kutegemea nchi wahisani,
       Amesema kwa sasa  amejipanga kuhakikisha anaziba mianya yote ya ukwepaji kodi ambayo ilikuwa inafanywa na wafanyabiashara wakubwa ambao walikuwa wanaikosesha mapato serikali kipindi cha nyuma kwa ukwepaji wa  kodi.
       Amebainisha kwa kusema kuwa kwa  sasa serikali haita wabuguzi wafanyabiashara ndogo ndogo kwa kuwakea mazingira magumu ambayo yalikuwa yanatokana na kodi zisizo za lazima huku akidai kwa sasa serikali ya awamu ya tano itawaangalia zaidi wafanya biashara wakubwa.
        Vilevile,Waziri Mpango amezitaka taasisi mbalimbali za kibenki kutanua matawi mbalimbali ya kibenk  hadi vijijini ili kuongeza uelewa akiba zao.
        Amesema  wananchi wengi waishio vijijini hawana uelewa wa kutunza pesa katika mabenk na wamekuwa na kasumba ya kutunza pesa katika  maeneo yasiyo stahiki ikiwemo nyumbani hivyo  ameahsa benk zitoe elimu ya kutosha kwa wananchi ili waweze kuwa na uelewa wa kutunza pesa hizo,
.kutunza   zilizopo nchini kuachana na ukasumba wa sasa wakutegemea mapato yake ndani ya mijini huku akiwataka kuwakea  

Hakuna maoni