Zinazobamba

NAIBU WAZIRI LUHAGA MPINA AWASHUKIA WATENDAJI NEMC,AWAPA SIKU 30 TU,SOMA HAPO KUJUA


Pichani ni Naibu Waziri wa Muungano na Mazingira,Luhaga Mpinaakizungumza na Watendaji wa Baraza la Mazingira NEMC pamoja wanahabari wote 
(hawapo pichani) mara alipofanya ziara kwenye Baraza hilo leo Jijini dar es Salaam


NA KAROLI VINSENT
NAIBU waziri wa Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina amewapa siku 30  viongozi wa Baraza la Mazingira nchini (NEMC),wawe wameshatoa hati 512 za wawekezaji waliotaka hati ya mazingira,
Hata hivyo ,amesema endapo agizo hilo lisipotekelezwa basi atamchukulia hatua mkurugenzi wa NEMC.
Naibu waziri Mpina ametoa kalipio  hilo leo Jijini Dar es Salaam wakiti alipofanya ziara katika makao mkuu ya NEMC ili kukagua kazi ya Baraza hilo ambapo amesema inasikitisha kuona wawekezaji wanakosa hati ya Tasmini ya athari ya Mazingira ambayo inampa ruhusu ya kuwekeza kwenye eneo,


Wanahabari wakimsikiliza Naibu Waziri



Amefafanua kuwa Sheria ya Maziringira mwaka 2004 inatoa mda wa siku 30 tu hati hiyo iwe imetolewa lakini Baraza hilo limetumia siku 90 bila kutoa hati hiyo jambo analodai kuwa limekuwa likiwakatisha tamaa wakezaji.
“nawapa siku 90 muwe mmetoa hati kwa hawa wawekezaji,naomba kabisa utekelezaji na sitaki kuja hapa tena nasikia habari hii ya hati,nawaambieni sitokuwa na msamaha nitamfukuza mkurugenzi ambayo kimamlaka naweza kufanya hivyo”amesema Naibu Waziri Mpina,
Sanjari na hayo Mpina amesema kwa sasa wapo mbioni kupeleka marekebisho ya sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 kwa kusema imepitwa na wakati kwani aiendani na wakati uliopo wamadiliko ya sayansi na teknolojia.

Ameitaja kasoro katika sheria hiyo ni tozo ndogo unazotoa kwa mtu anayekiuka sheria hiyo ,jambo analodai limechangia watu wengi kupuuza tozi hiyo na kuendelea kuharibu mazingira.
Pichani ni Naibu Waziri akiwa na picha ya pamoja na viongozi wa NEMC

Hakuna maoni