Zinazobamba

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TMA YAZINDUA MFUMO BORA,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni mkurugenzi wa TMA,Dkt  Agnes Kijazi

MAMLAKA ya hali hewa nchini (TMA) kwa kushirikiana na kituo  cha kimataifa cha Utafiti  kilichopo Marekani “Internation  Reseach Institute (IRI) kwa pamoja wamezindua mfumo utakao wawezesha  watumiaji wa huduma za  hizo kuzipata kupitia mtandao wa (TMA).Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
          Akizindua mfumo huo  leo jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka  DktBurahani Nyezi aliitaka Mamlaka ya hali ya hewa  kuongea ufanisi  katika utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini,
       Aidha,Dkta Nyezi  ameipongeza TMA kwa jitihada  zake za kushirikiana na wataalamu  kutoka nchi mbali mbali ambazo  ni wanachama wa shirika la hali hewa duniani katika kuboresha hali hewa nchini,
            Vilevile Mwenyekiti huyo wa Bodi ya Ushauri TMA aliishukuru kituo cha kimataifa cha (IRI) kwa msaada waliotia pamoja na kuiwezesha TMA kukamilisha mfumohuo na kufikia hatua ya kuzinduliwa rasmi,
Kwa upande wake mkurugenzi wa TMA,Dkt  Agnes Kijazi alitoa msisitizo kwa wadau kuzingatia matumizi sahihi ya taarifa za hali hewa ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli za kiuchumi na kijamii na pia kuweza kukabiliana na majanga  yatokanayo na  hali mbaya ya hewa.


Hakuna maoni