NAFASI YA UWAZIRI MKUU YAIPASUA KAMBI YA MAGUFULI,JANUARY MAKAMBA NA MWIGULU WAJIAPIZA,SOMA HAPO KUJUA

NAFASI ya Uwaziri mkuu endapo Mgombea Urais kupitia
Chama cha Mapinduzi CCM,john Magufuli akiwafanikiwa kuwa Rais wa awamu ya
tano,imetajwa kukigawa chama hicho makundi mawili.(Mtandao huu umedokezwa),Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo.
Taarifa
za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata kutoka ndani ya Kamati ya ushindi ya
CCM,zinasema kumeibuka makundi mawili yanayopambana kufa na kupona kuhakikisha
wanateuliwa kushika nafasi hiyo kubwa Serikalini,
Chanzo chetu hicho
kinasema makundi mawili hayo ni moja likiongozwa na January Makamba
pamoja na Kundi jengine linaloongozwa na Mwigulu Nchemba ambao wote kwa pamoja
wanajiapiza kuteuliwa nafasi ya Uwaziri mkuu.
“Ujue
sahivi hawa mabwana (January na Mwigulu) wamekigawa chama ndugu,leo wanajiona
kama wao ndio wenye chama,wanajiapiza kuwa lazima washike nafasi ya uwaziri
mkuu,yaani wamekuwa na kiburi cha ajabu mpaka tunashangaa”amesema chanzo chetu
hicho.
Kuibuka
kwa taarifa hizi kunakuja ikiwa imebaki siku nane kabla ya uchaguzi mkuu
kufanyika hapo octoba 25,kwa mujibu wa marafiki wa Karibu wa Januray Makamba
ambaye ni msemaji wa Kamati ya Ushindi,wamesema ni kwamba Makamba
ameshajihakikishia asilimia 100 kuwa yeye ni waziri mkuu kwenye Serikali ya
Magufuli.
“Sikufichi
hizi taarifa ni za kweli maana January Makamba amekuwa akijihamini kwamba
lazima awe waziri mkuu,bira hata sisi kutuambia sababu ya yeye kujiamini huku
ikizingatia hata kabla ya uchaguzi mkuu,kufanyika bado,”
Mbali na
Makamba na Mwigulu,makada wengine wa CCM
wanaojiapiza lazima washike nafasi hiyo ni Wiliam Lukuvi,pamoja na Dk Mwakyembe
ambao wote inatajwa pia wanainyemelea nasafi hiyo.
No comments
Post a Comment