TCRA WAZINDUA ZOEZI LA UHAKIKI NA USAJIRI WA LAINI ZA SIMU,WATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KUHAKIKI LAINI ZAO
| Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa mamlaka ya vitambulisho NIDA Bw. Thomas William akielezea jambo kuhusu umuhimu wa kitambulisho cha taifa na zoezi la kuhakiki laini za simu. Wiliam alisema vitambulisho vya taifa vina taarifa za kuaminika na sahihi za kila mkazi wa Tanzania na ndio sababu inapendkezwa kutimika katika zoezi hili. |
Mamlaka ya
mawasiliana Tcra imetangaza kuzindua rasmi zoezi la kuhakiki na kusajiri laini
za simu kwa kutumia mfumo mpya kabisa wa kidijitali Kupitia Smart Phone kwa
Programu ya KYC
Akitangaza
kuanza kwa zoezi hilo (validation of sim card) Prof. Nkoma alisema wananchi
wanapaswa kujitokeza kwenda kuhakiki laini zao ili kuendelea kujipatia
huduma zilizo bora kupitia laini zao ambazo zimesajiriwa kihalali.
Alisema zoezi hilo
litaendeshwa kwa njia ya Mtandao, ambapo mawakala watatumia simu ya mkononi aia
ya smatphone ili kujaza taarifa za uhakiki wa laini pamoja na usajiri ambao
vitaenda sambamba.
Aliongeza kusema
ujio wa zoezi hilo ni la kawaida ambapo hata benki kuu ya Tanzania BOT iliwahi
kuagiza benki mbalimbali hapa nchini kufanya uhakiki wa akaunti za wateja wao
ili kuwa na taarifa muhumu za wateja
Akizungumzia jinsi
zoezi litakavyo tekelezwa, Prof Nkoma alisema makampuni ya simu watatumia
mawakala wao kusajiri na kuhakiki wateja ambao tayari wamesajiriwaa kwa kutumia
smatphone ambazo zitagawiwa kwao ili kutekeleza kazi hiyo muhimu.
Alisema mteja
atalazimika kuwa na kitambulisho cha taifa ili afanyiwe uhakiki,na kwamba kwa
wale ambao kwa kiasi kikubwa hawana wafanye jitihada ya kutafuta kitambulisho
hicho ambacho kwa sasa alidai kinapatikana ndani ya siku saba.
Teknolojia hiyo
mpya inauwezo wa kutambua kitambulisho bandia, uwezo wa kupiga picha, kupiga
picha ya kitambulisho, kutia saini zote mbili ya mteja na wakala, na kujaza taarifa
muhimu za mteja, na kwamba inafanya kazi hizo kwa haraka na uhakika.
No comments
Post a Comment