Zinazobamba

HATIMAYE SASA,MZEE YUSUPH KUGOMBANIA UBUNGE,SOMA HAPA KUJUA JIMBO GANI

yus
PICHANI NI MZEE YUSUPH PICHA NA MAKTABA
MSANII wa Muziki wa Taarabu kutoka Bendi ya Jahazi Modern Taarabu ,Mzee Yusuph anatalajia kugombania Ubunge kupitia Jimbo la Fuoni lilopo Unguja kwa kupitia CCM,Mtandao huu umedokezwa,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
         Mzee Yusuph ambaye ni Mwazilishi wa Taarabu za Mfumo wa Modern nchini atalajia kuchukua fomu mda wowote kutoka sasa na kumpiku Mbunge wa sasa wa Jimbo hilo,Said Mussa Zuberi.
        Kwa Mujibu wa Mzee Yusuph  ambaye pia ni Mmiliki wa Bendi ya Jahazi,anasema lengo la yeye kugombani Ubunge  Jimbo hilo ni kutaka kuwaleta maendeleo kwa Wananchi wa Fuoni pamoja na Wazanzibari kwa Ujumla..
       Pamoja na hayo Msanii huyo wa Zamani wa Bendi ya  Zanzibar Melody Taarabu amewataka Wananchi wa Jimbo hilo kumuunga mkono kwani yeye ni mtu sahihi ambaye anaweza kuwaleta Maendeleo Makubwa.

  Kuibuka kwa Mzee Yusuph kunazidisha idadi ya Wasanii wa Muziki ambao wanatarajia kugombania nafasi mbali mbali za uongozi kwenye uchaguzi Mkuu wa hapo baadae mwaka huu, baada ya Hivi Karibuni Msanii wa Bongo fleva,Profesa Jay kutangaza Rasmi kuombania Ubunge Jimbo la Mikumi kupitia muunganiko wa Vyama vikuu vya Upinzani vinavyounda UKAWA.

Hakuna maoni