Zinazobamba

MAKADA WA CCM WAGOMBANIA IKULU,WASIRA,MWIGULU NAO WAJITOSA,VIJEMBE VYATAWALA,SOMA HAPO KUJUA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.
Pichani ni Steven Wassira ambaye leo ametanga Rasm kuwania Urais ndani ya CCM

WIMBI la Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM,kugombania nafasi ya  kumrithi Rais anayemaliza Mda wake Jakaya kikwete hapo baadaye mwaka huu, limezidi kuongezeka huku Makada hao  wakiweka Vijembe na majungu vikitawala. Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo.
    Mlango huo ulifunguliwa jana na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwenye Kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound Edward Lowassa nyumbani kwake Arusha na kutangaza Safari ya matumaini ambayo yenye Ajenda ya kutaka Urais.
        Hatimaye leo wameibuka Makada wengine wa Chama hicho kikongwe barani Afrika kilichopo madarakani na kutangaza kutaka Urais huko wakiweka Sera ambazo wanadai zitamsaidia mtanzania.
         Makada hao ni Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu  Nchemba ambaye naye amejitokeza na kutaka Urais huku akiweka Vipaumbele mbali mbali pindi atakapopitishwa na  CCM.
        Akitangaza azma hiyo Kwenye Chuo kikuu cha Mipango mkoani Dodoma huku akishuhudiwa na mamia ya Watanzania amesema nia ya Sababu iliyomsukuma kuitaka nafasi hiyo kubwa inatokana na kushuhudia watanzania wakiteseka na Umasikini huku wakiwa na Rasilimali lukuki.
“Mimi mwenyewe umasikini naujua maana nilipomaliza shahada yangu ya pili pale Chuo kikuu nilikuwa masikini sina kazi,harafu nilikuwa nimeoa nikaamuna kujiingiza hata kwenye kazi za kubeba zege ,ndio maana naitaji nafasi ya Urais kwa lengo la kuwasaidia watanzania ambao wamekumba na umasikini lukuki”
        Pamoja na hayo Mwigulu akusita kuzungumzia suala la kilimo ambapo amesema akipata nafasi hiyo atatumia kila njia kuweka kuongeza viwanda ndani ya nchi ili kuweza kumuokoa mkulima pindi atakapouza mazao yake.
       Sanjari na Mwigulu Nchemba kuibuka kutaka Urais, hapo mwanzo pia mwengine ni Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Steven Wasira ambapo nae ametangaza Rasmi kuitaka nafasi ya Urais na kusema pindi akipewa nafasi atainua sekta ya Kilimo ambayo anadai ni uti wa mgongo.
           VIJEMBE VYA TAWALA.
Licha ya Makada hao watatu kutangaza nafasi hiyo Vijembe vilitawala vya kupondana wao kwa wao.
        Lowassa
Wa kwanza kurisha Vijembe alikuwa ni Waziri Mkuu Aliyejiuzulu Edward lowassa ambaye amesema anashangaa watu wanaoutaka Urais huku hata awajakaa madarakani kwa mda mrefu.
“Mimi nimpigana kwenye Vita vya Iddi Amin najua changamoto zake tena ni nauzoefu hebu waulizeni hao wengine wanamiaka michache harafu anautaka Urais”amesema Lowassa
       Mwigulu ajibu kijembe hicho
   “unaweza kukaa madarakani kwa mda mrefu watu wanaangalia umefanya nini?kwasababu unaweza kukaa mda mrefu Serikalini huku ukaitia Serikali hasara ya Mabilioni ya pesa”amesema Mwigulu



Hakuna maoni