Zinazobamba

WAZIRI MWAKYEMBE ALIPUKA,AJIPANGA KUWAFUKUZA MAHAKIMU WENYE CHETI NA DIPLOMA,KISA NI HICHI HAPA,SOMA HAPO KUJUA

Waziri  wa katiba na sheria Mh. Dkt Harrison Mwakyembe amesema serikali itawafuta kazi mahakimu wote wa mahakama ya mwanzo wenye elimu ya cheti na diploma ya sheria.
“Tunahitaji mahakimu wenye uwezo wa sheria ambao wamehitimu shahada ya kwanza,hivyo serikali itawafuta kazi mahakimu wote wenye elimu ya cheti na diploma” 
Dkt mwakyembe ameyasema hayo leo jijini dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mswada wa sheria ya msaada wa kisheria ambapo amewaomba wananchi na wadau wa sheria nchini kufanyia mapitio mswada huo na kutoa maoni yao kwa kamati ya bunge ya katiba na sheria wakati utakapowadia.
Dkt mwakyembe amesema bunge litaweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kupokea maoni ya wadau wote watakaofika mbele ya kamati na wale watakao wasilisha maoni yao kwa njia ya maandishi.

Aidha waziri mwakyembe ameelezea mswada huo ambao umesomwa bungeni kwa mara ya kwanza tarehe 10 novemba utawatambua watoa huduma za msaada wa kisheria na utakuwa ni ukombozi kwa jamii ya watanzania walio wengi ambao hushindwa kumudu gharama za kuwalipa mawakili.