Zinazobamba

AKILI YA MBUNGE KUBENEA JIMBONI KWAKWE,MWILI WAKE BUNGENI,TIZAMA ALICHOFANYA KWA WANANCHI WAKE,SOMA HAPO KUJUA




Balozi wa Kuwait aliyevaa kanzu, Jasem Alnajen akiwa amefungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua kisima cha maji kilichojengwa kwa msaada wa nchi hiyo eneo la Golani, Kimara jijini Dar es Salaam, jana kupunguza adha ya shida ya maji. Kushoto ni Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea na kulia ni Diwani wa Kata ya Kimara, Paschal Manota.
Balozi wa Kuwait aliyevaa kanzu, Jasem Alnajen akiwa amefungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua kisima cha maji kilichojengwa kwa msaada wa nchi hiyo eneo la Golani, Kimara jijini Dar es Salaam, jana kupunguza adha ya shida ya maji. Kushoto ni Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea na kulia ni Diwani wa Kata ya Kimara, Paschal Manota.

WANANCHI wa Golani, Kimara katika Jimbo la Ubungo, jijini Dar es Salaam wamemshukuru Saed Kubenea, mbunge wa jimbo hilo kwa kuwasaidia kupata kisima cha maji, anaripoti Regina Mkonde.

Wametoa shukurani hizo wakati Jasem Alnajen, Balozi wa Kuwait nchini Tanzania akikabidhi kisima cha maji kwa Kubenea kwenye eneo hilo.

“Tulikuwa na shida kubwa ya maji hapa, kwa hakika huu ni msaada mkubwa kwetu. Tunamshukuru mbunge wetu kusaidia upatikanaji wa kisima hiki,” ameeleza Beatrice Samweli, Mkazi wa Kimara.
Hata hivyo, Kubenea amemuomba Balozi Alnajen kuwa mlezi wa eneo hilo sambamba na kuendelea kutoa  misaada mbalimbali jambo ambalo ameridhia.

Miongoni mwa shughuli alizokubali serikali yake ya Kuwait kusaidia eneo hilo ni ujenzi wa shule, zahanati, ukarabati wa barabara, kumalizia msikiti  ikiwemo uchimbaji wa visima vingine vitano.

Wakati akipokea kisima hicho Kubenea alimshukuru balozi huyo na kuwaeleza wananchi hao kwamba, jitihada hizo zimetokana na ahadi aliyotoa ya kuwapunguzia tatizo la maji katika eneo hilo.
Amewataka wananchi hao kuhifadhi kisima hicho ambacho kitakuwa  mwanzo wa visima vingine katika kampeni ya kumaliza tatizo la maji ambalo limekuwa kwa muda mrefu.

Hakuna maoni