BILIONEA LUGUMI NI KIBURI,AWAKIMBIA WAANDISHI WA HABARI ALIOPANGA KUKUTANA NAO,AZIDI ICHEZEA SHARUBU SERIKALI YA MAGUFULI,

SAID Lugumi ambaye ni
mmiliki wa Kampuni ya Lugumi Enterprises ambayo imengia mkataba tata wa zaidi
bilioni 37 na Jeshi la Polisi nchini mmilikihuyo amezidionyesha umwamba wake
baada ya kuwakimbia waandishi wa Habari ambao alipanga kukutana nao.Anaadika
KAROLI VINSENT endelea nayo.
Tukio hilo la aina
yake limetokea leo Jijini Dar es Salaam,ambapo Lugumi alitakiwa kuongea na
waandishi wa habari katika ofisi yake majira ya saa sita
mchana,ambapo waandishi wa habari kutoka vyombo tofauti vya habari
walijitokeza,
Mara baada ya mda huo
wa kuanza mkutano kufika,Lugumi naye alikuwa hajafika,ndipo wanahabari
wakasubili mpaka kufika saa saba mchana ndio akajitokeza msemaji wa Kampuni ya
Lugumi aliyejitamburisha kwa jina Jumma Moshy Sabury na kuwaambiana wanahabari Lugumi amepata
safari ya ghafla.
“Jamani Lugumi
hataweza kuja kwenye mkutano huu,kwani
amepata safari ya ghafla na ameenda Dodoma kukutana na wabunge kuzungumza nao,”amesema
Sabury.
Licha Sabury kusema
haya,akatoa Tamko ambalo amedai limetoka kwa Lugumi,huku tamko hilo likiwa
linatolea ufafanuzi kuhusu taarifa zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari.
Tamko hilo lenye
kurasa mbili licha ya kukanusha kuwa mkataba wa lugumi kuwa ni wa halali pia Tamko
hilo lilishindwa kuonyesha sababu ya Kampuni hiyo kushindwa kumaliza
ufungaji mashine za kuchukua alama za vidole katika
vituo vya polisi 108 nchi nzima huku akifunga mashine 14 tu,wakati
amelipwa asilimia 99 ya malipo yote ambazo ni bilioni 34,
Jambo lilowafanya
Waandishi wa Habari kumuliza msemaji huyo lakini alishindwa kutolea ufafanuzi.
WANAHABARI WANENA.
Akizungumza kwa
kujiamini Mmiliki wa blog ya Fullshangwe, John Bukuku amesema
Lugumi anachezea akili za Watanzania
Amesema kama kweli alikuwa na safari ya kwenda Dodoma kulikuwa na haja gani ya kuita mkutano na waandishi wa habari.
Kinachooneka hapo ni kwamba Lugumi ameamua makusudi kuwakimbia waandishi wa habari akijua wazi asingeweza kujibu maswali yao.
."Yaani kama kuna siku Kampuni ya Lugumi Imechemsha basi ni leo, kuwakimbia wanahabari sio mwisho wa matatizo badala yake itazidi kuongeza tatizoa"Alisema Bukuku.
Naye Mmiliki wa Fatherkidevu blog amesema ameshangazwa kuona mmiliki wa Kampuni hiyo anatoa nakala kwa waandishi wa habari badala ya kuja kujibu hoja za msingi anazotuhumiwa.
Amesema wanahabari walitarajia angejitokeza kuja kupangua hoja mbalimbali ambazo zinachafua kampuni yake lakini imekuwa kinyume chake
Amesema kama kweli alikuwa na safari ya kwenda Dodoma kulikuwa na haja gani ya kuita mkutano na waandishi wa habari.
Kinachooneka hapo ni kwamba Lugumi ameamua makusudi kuwakimbia waandishi wa habari akijua wazi asingeweza kujibu maswali yao.
."Yaani kama kuna siku Kampuni ya Lugumi Imechemsha basi ni leo, kuwakimbia wanahabari sio mwisho wa matatizo badala yake itazidi kuongeza tatizoa"Alisema Bukuku.
Naye Mmiliki wa Fatherkidevu blog amesema ameshangazwa kuona mmiliki wa Kampuni hiyo anatoa nakala kwa waandishi wa habari badala ya kuja kujibu hoja za msingi anazotuhumiwa.
Amesema wanahabari walitarajia angejitokeza kuja kupangua hoja mbalimbali ambazo zinachafua kampuni yake lakini imekuwa kinyume chake
UTATA WA KAMPUNI YA LUGUMI.
Katika mkataba huo, Kampuni ya Lugumi ililipwa
kiasi Sh bilioni 34 ambazo ni sawa na asilimia 99 ya fedha za makubaliano ya
mkataba, lakini hadi sasa mashine hizo zimefungwa katika vituo 14 pekee jijini
Dar es Salaam ambavyo hata hivyo haijaainishwa maeneo vilipo,kwa mujibu wa
taarifa mbali mbali zinasema kati ya mashine hizo 14 ni mbili tu zinazofanya
kazi.
Mkataba huo wa Polisi na Lugumi umezidi kuchukua sura mpya
baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kunyang’nywa hoja hiyo na
badala yake kuhamishiwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na
Usalama.
Hatua hiyo inatokana na utata uliogubika mkataba huo ambao
unawahusisha vigogo kadhaa wa Jeshi la Polisi pamoja na baadhi ya watendaji wa
Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, huku ikidaiwa kuwa huenda ikawa njia ya
‘kulindwa’.
Kutokana na hali hiyo, hadi kufikia Jumatatu saa 10 jioni, Makamu
Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly, alisema kuwa kamati yao haijapokea taarifa
yoyote kuhusu Kampuni ya Lugumi, ambapo kamati hiyo ililitaka Jeshi la Polisi
kuwasilisha mkataba huo
Post Comment
Hakuna maoni
Chapisha Maoni