Zinazobamba

DOKTA SLAA KUUMBULIWA KILA KONA,TEC WAJIPANGA KUMJIBU ,SOMA HAPO KUJUA



SIKU moja kupita baada ya Aliyekuwa Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Dk Wilbroad Slaa kuwatuhumu maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini kupokea rushwa kutoka kwa mgombea wa Urais kupita Chadema Edward lowassa ,
Ambapo  sasa  Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limechukizwa na tuhuma hizo na mda wowote kutoka sasa wanajiandaa kutoa tamko kali kwa kupinga tuhumu hizo.
       Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu  aliyoko ndani ya Baraza hilo ameuambia mtandao huu kuwa wako mbioni kuweka sawa taarifa hizo.
     Amesema TEC hawatafumbia habari zozote zitoelewazo kwa jamii zenye kuleta utofauti wa kimitazamo na kupanga kutoa taarifa ya ukweli ili jamii ijue,. 
      “Kusema kweli hata hizi taarifa tumezisikia na sisi,yaani hatutegemea kabisa mtu ambaye anahaminika kama Dk Slaa kuongea mambo kiajabu kama vile,kama anasema kuna maaskofu 30 wamehongwa ni vema angewataja,lakini amekaa kimya basi na sisi tutatoa tamko kwenu kuhusu hali hiyo maana kauli hizi zinakuwa zinautata”kimesema Chanzo hicho.
         Dk Slaa ambaye kihostoria aliwai kuwa Padri wa kanisa Katoliki alitangaza kile anachodai ni kununja ukimwa uliokuwa umetanda juu ya hatma yake ndani ya Chadema huku akiwaambia waandishi wa Habari jana kwenye hoteli moja hapa jijini alisema sababu ya kuachana na Chadema pamoja na kuachana na siasa inatokana kile anachoiita ni kupuuzwa  kuhusu hatua ya kumkaribisha Lowassa.
UTATA WA MKUTANO WAKE NA WANAHABARI.

      Mwandishi wa Mtandao alifika kwenye hoteli ya serena jijini dare s Salaam na kushuhudia umati wa waandishi wengi ambao tofauti na kawaida,wakati waandishi wa Habari wakisubili mkutano huo kuanza ,ukumbi Kote Kulizungukwa na watu wanaozaniwa kuwa ni wa Idara ya Usalama wa Taifa huku ikizidisha mashaka uwepo wa watu wale pale.
        Wakati Slaa anawasili kwenye mkutano huo aliongoza na Mhariri moja wa Gazeti linalotoka mara moja kwa wiki huku akiongozana  pia na watu wanaozania kuwa ni usalama wa Taifa  waikifikia saba.
        Wakizungumia hali hiyo baadhi ya waandishi wa habari waliokuwepo katika mkutano huo, waliumbia mtandao huu kuwa mkutano huo uwenda ulikuwa na malengo tofauti ya kisiasa kwani uwepo wa usalama Taifa hao unatilia shaka.
“Yaani hata sisi tunashangaa hawa wanaozaniwa ni usalama wa Taifa wapo kwenye mkutano na wanahabari, harafu  wanapigia makofi anachozungumza Slaa,tena mbaya zaidi huyuhuyu Slaa wakati yupo chadema alikuwa anawatuhumu watu hawa kuwa walikuwa wanataka kumdhuru,sasa inakuwaje huyu huyu  leo analindwa na hawa hawa alikuwa wanatuhumu watanzania wawe makini”


Hakuna maoni