Zinazobamba

WAZIRI SITTA AMLIPUA ZITTO KABWE,NI KUHUSU RUGEMALIRA,AMESEMA NI MUONGO NA MPOTOSHAJI SOMA HAPA KUJUA


NA KAROLI VINSENT
Siku chache kupita baada ya Kiongozi Mkuu wa Chama cha siasa  ACT-Wazalendo Zitto Kabwe (pichani) kifichua kile anachodai ni ufisadi unaofanywa na Serikali kwa kitendo chake cha kumpa tenda Mkurugenzi wa VP Engineering Bwana James Rugimalira kwenye Ujenzi wa Reli kutoka Mwambani Tanga hadi nchini Kongo kwa kudai  kumegubikwa na ukiukwaji wa kanuni kutokana na kutotangazwa tenda hiyo kwa umma.
        Naye Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta ameibuka na kumvaa mwanasiasa huyo na kusema amejaa uongo na ni mpotoshaji kwani serikali haihusika na mradi huo na wala haijatoa fedha kumpa bwana Rugimalira.
          Kauli hiyo ya Waziri Sitta ameitoa leo Jijini Dar es Salaam wa wakati wa Mkuano na waandishi wa Habari ambapo amesema inasikitisha kuona mwanasiasa anataka kujijenga kisiasa kupitia kwenye mambo anayodai ni ya uongo,kwani mradi ambao anafanya bwana Rugimalira ni mpango wakwao  kwenye sekta binafsi.
        “Kwanza hakuna ufisadi wowote kinachotokea kule mwambani Tanga ni watu wa sekta binafsi wanabuni mitaji  na Rugimalira ndio anafanya hivyo kwa kushirikiana na shirika la Maendelea (NDC)wanakuwa wanakibuni mitaji baadae  kuja kutuletea serikali na sisi tunaweza kukubali au la”amesema Waziri Sitta
        Waziri Sitta ameongeza kuwa kitendo anachosema kwamba Serikali imehusika kutoa fedha zake sio kweli na amesema  uhenda Mbunge huyo wa zamani wa Kigoma alikuwa ataka umaarufu tu wakisiasa.
         Amebainishwa kuwa na hata katika hatua za awali teyari Serikali ilikuwa imeukataa mradi wenyewe wa Reli kwa kuwa wamebaini  hautawezi kuinufaisha nchini kwakuwa sehemu kubwa ya Reli itajengwa nje ya nchi ambayo ni nchi ya Kongo.

       “Harafu tena katika hatua za awali tumesema hatuwezi kukubali kabisa kuhuruhusu huo mradi tuuchukue serikali kwani hatuwezi kunufaika nao kwakuwa sehemu kubwa ya reli inajengwa nje ya nchi na sehemu ndogo tu ndio tunanufaika watanzania achia mbali sehemu ndogo pia sisi tayari pale tanga kuna Reli ipo hatuwezi kuuchukua mradi huo “amebainisha Waziri Sitta. 

No comments