HALI YA CHAKULA NCHINI NI SHWALI,WAZIRI WASIRA ASEMA SERIKALI IMEJIPANGA KUPAMBANA NA NJAA,SOMA HAPA KUJUA
![]() |
| pichani ni Waziri wa Kilimo,Ushirika na Chakula Steven Wasia akifafanua jambo na waandishi wa Habari picha na Maktaba |
SERIKALI
nchini imesema hali ya chakula katika maeneo mengi ya nchi kati ya mwaka 2014
na 2015 imeendelea kuwa imara kufuatia mavuno mazuri yaliyopatikana msimu wa
kilimo katika kipindi hicho.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Hayo yametengazwa leo Jijini Dar es
Salaam na Waziri wa Kilimo na Chakula na Ushirika Steven Wasira wakati wa
Mkutano na vyombo mbali mbali vya Habari ambapo amesema kulingana na Tathmini
ya uzalishaji uliofanyika mwezi Agosti 2014 uzalishaji wa mazao ya chakula
katika msimu wa mwaka 2013 na 2014 ulifikia tani 16,015,238 zikiwemo tani
9,828440 za nafaka.
Waziri Wasira ameongeza kuwa mazao
yasiyo na nafaka yalikuwa tani 6,186,698,kwa
mujibu waziri anasema uzalishaji huo ukulinganisha na mahitaji ya chakula ya
tani 12,767,979 kwa mwaka 2014/2015.nchi ilikuwa na zaidi ya tani 3,247,359 za
chakula ya ziada ya mahindi ambayo ilikuwa ni tani 1,547.570 na mchele ilikuwa
tani 794,192.
Amebainisha kuwa nchi ilijitosheleza
kwa chakula kwa asilimia 125 ambapo,mikoa 23 kati ya 25 Tanzania bara
ilibainika kuwa na kiwango vya ama ziada au utoshelevu na mikoa miwili tu
ilidhihilika kuwa na uhaba wa chakula.
Katika hatua nyingine Waziri Wasira
amesema katika kipindi kinachoendelea cha Mwaka huu na mwaka 2016 kutarajiwa
kuwa na uhaba wa chakula katika mikoa ya 10 ambayo imeoneka kutopata mvua
kabisa ambazo anadai zimewakwamisha wakulima kufanya shughuli za kilimo.
Waziri Wasira aliitaja mikoa hiyo ni Arusha,Kilimanjaro,Manyara,Shinyanga,simiyu,Tabora,Mara,Kagera,Lindi
Mtwara,morogoro,singina na katavi.
Ambapo amesema jitihadi za Serikali
ilizochukua katika mikoa hiyo ni kupeleka Chakula cha kutosha ili kuondoa
Tatizo hilo.
Vilevile Waziri Wasira amewataka
wakulima kutunza akiba ya chakula ili
kujihami na balaa la njaa ambalo linaweza kutokea mbeleni.
.jpg)
No comments
Post a Comment