Zinazobamba

MAGAZETI YA MENGI YATIA FORA KWENYE TUZO ZA WANAHABARI SOMA HAPA KUJUA

Magazeti yakiwa mezani yanauzwa

VYOMBO vya Habari vinavyomilikiwa na kampuni ya (IPP Media)vimetia fora kwenye Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari nchi baada ya vyombo hivyo kutoa waandishi wengi katika tuzo hizo.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
          Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu mtendaji na mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tuzo za uandishi wa Habari mwaka huu Kajubi d Mukajanga wakati wa mkutano na vyombo mbalimbali vya Habari ambapo amesema katika tuzo za mwaka katika waandishi waliopeleka kazi walizofanya ili zishindaniwe na baadae kutangazwa mshindi vyomba vya habari vya (IPP Media) vimekuwa kinala.
       Bwana Mwakajanga alivitaja vyombo hivyo vya ni Gazeti la kingereza la The Guardian ambapo waandishi wake wamepelea kazi zazo kuhindaniwa ni 137 na kufuatiwa na Gazeti la mwananchi ambao nao waandishi wake wamepeleka kazi 87.
       Mbali na Mwananchi chombo kingine cha Habari kilichopeleka kazi nyingi ni Afya Redio nayo pia waandishi wake wamepeleka kazi nyingi zikiwa 68.
       Aidha,Mwakajanga amesema kwa sasa hatua iliyobaki ni kwa majaji wa walioteuliwa na kamati hiyo ili kuzipitia  na kuchaguliwa mshindi ambaye atangazwa kwenye hafla fupi hivi karibuni

No comments