Zinazobamba

KIFO CHA KOMBA,WANASIASA WAMLILIA,DOKTA SLAA ASEMA YAMOYONI,SOMA HAPA KUJUA


SAA chache kupita baada ya Mbunge wa Mbinga mashariki Kaptain John Komba kufaliki Dunia Gafla kutoka na kusumbuliwa na Ugonjwa wa kisukari kwa mda mrefu , Viongozi mbalimbali wakimwemo wanasiasa wametoa masikitiko yao kufuatia kifo hicho.Anaripoti KAROLI VINSENT endelea nayo hapo.
             Wakizungumza na Blogs hii kwa wakati mmoja wanasiasa hao wameonyesha kugushwa na msiba huo, na Wakwanza aliyezungumza na mwandishi wa Habari hii ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa amesema kifupi yeye mwenyewe amepata taarifa hizi kupitia mitandao  ya kijaa na imemsikitisha sana.
     “Kikukweli mimi mwenyewe nimepata taarifa hizi kwenye mitandao mbalimbali cha kwanza imenisikitisha sana,kwani Komba ni miongoni mwanasiasa waliolijenga taifa hili changa kwa mafanikioa makubwa sana”amesema Dokta Slaa.
         Dokta Slaa ameongeza kuwa  anatumia nafasi hii kutoa pole kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Jakaya Kikwete  ambacho ndicho chama  Komba anatoka kwa msiba huo mkubwa, na akawataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.
              Naye Mwenyekiti asiyetambulika na Msajili wa Vyama vya Kisiasa nchini kutoka chama cha ACT-Tanzania Kadawi Limbu naye ametoa pole kwa chama cha Mapinduzi CCM kwa msiba huo pamoja na Wasanii kwa ujumla na akisema Taifa maendeleo.
             Kwa Upande wake Mwandishi wa Habari Mwandamizi kutoka kituo Cha Chanel Ten pamoja na Radio ya Magic Fm Kibwana Dachi naye ameonyesha masikitiko yake baada ya kutokeo kwa kifo hicho na Kusema ni pigo kubwa sana kwa Taifa.

            “ Kifo cha Komba  kimenisikitisha sana na hata kwa watanzania wote hususani sisi waandishi wa habari kwani ni   mtu  aliyeijenga jamii ya kisiasa kwa kutumia maono mazuri,na hata pia katika sanaa ni mtu aliyerudisha mfumo wa uimbaji kwa kutumia mfumo wa kwaya yaani kwa kifupi naweza kusema ni pengo kubwa sana kwa taifa”amesema Dachi

Hakuna maoni