Zinazobamba

DC MAKONDA AANZA KAZI KWA MIKWALA MIZITO SOMA HAPA KUJUA

Pichani ni Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni
Paul Makonda


MKUU mpya wa wilaya ya Manispaa  Kinondoni Paul Makonda ameapa kufa na matajili pamoja na viongozi mbalimbali waliovamia maeneo ya wazi na kujimilikisha kinyume na sheria.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo.
        Makonda ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari mara baadya ya kukagua shule za msingi zilizopo kata ya Tandale Ambapo Makonda amesema hatokubali kuona watu wanaojiita matajili ambao wameshirikiana na viongozi wa Halmashauri  katika kuwapora wananchi maeneo ya wazi na kujimilikisha huku wananchi wakihangaika .
          “Nawapa salam kabisa viongozi wa Halmashauri  ambao wameshirikiana na matajili ili kupora maeneo ya wazi ambayo yapo   kwa ajili ya viwanja vya michezo lakini viongozi warafi wa halmshauri wameona sahihi kuwapora  viwanja,nasema sitokubali kabisa,nawapa salam lazima viwanja virudi na atakaye kaidi basi nitakuja kuvunja na polisi wangu”amesema Makonda.
           Makonda ameongeza kuwa tatizo la migogoro ya Ardhi ataliweka kipaumbele katika wilaya hiyo ili kuweza kumaliza na ikiwezekana kuondokana na tatizo hilo.

       Aidha,Makonda amewataka wananchi wa manispaa ya kinondoni wampe ushirikiana ili kuweze kuiweka manispaa hiyo katika hali nzuri ya kimaendeleo.

Hakuna maoni