VITI VIKIWA TUPU BAADA YA WADAU KUTUPIANA KATIKA MKUTANO HUO, MAJERUHI WANADAIWA KUTOWEKA NA KUSHINDWA KUELEWA WAPI WALIPOPOTELEA.
Vyama vya Siasa viliitisha maandamano yakadhibitiwa na Polisi, Bungeni
walilindwa na Polisi wenye farasi na magari ya deraya. Mimi naanza
kushawishika kwamba safari ya CCM ndio sasa imeiva maana hata farao
alipoona wana wa Israel alitumia mbinu na mabavu kama wafanyavyo CCM leo
hii.
Mfalme Sauli alipokwisha nyang'anywa upako wa utawala ilimlazimu
kumwinda kijana Daudi usiku na mchana akidhani nguvu zake zitabadili
mtazamo wa Mungu. Kama ilivyoandikwa kwenye maandiko Kitabu Kitakatifu
kuhusu Mfalme Belishaza alioona Maandiko yameandikwa ukutani akashindwa
kuyasoma, akawatafuta waganga, nao wakashindwa kuyasoma ndipo akamwita
Daniel.
Anachokieleza Jaji Joseph Sinde Waryoba watu wote wa CCM hawawezi
kukielewa hata kama mtatumia maguvu kiasi gani. Watakachoweza kukielewa
ni deal za Ufisadi, matumizi ya waganga kama walivyoletwa kwenye Bunge
la Katiba, na kule walikokimbilia wakati wa Babu wa Lodiondo kwenye
Kikombe.
Mzee Waryoba tunakuombea kwa Mungu uendelee na kazi hii ya manufaa kwa
wanyonge. Ikumbukwe kwamba Ninyi watu wa Mkoa wa MARA ndio waasisi wa
Ukombozi na Uhuru wa wanyonge. Mwalimu alijitolea maisha yake yote
hakuwa mtu mbinafsi. Tunaamini sasa kupitia kwenye taasisi ya Mwalimu
Nyerere na ninyi wazee wetu wenye maisha manyoofu ambayo hayana tuhuma
zozote kuhusu ufisadi, rushwa na ukandamizaji.
Tunaomba Mfuko wa Mwalimu Nyerere utoe namba za AKAUNTI ili watanzania
wenye kuchoshwa na UKOLONI wa CCM wachangie ukombozi ili mwende kila
kona ya nchi hii kutoa elimu hii ya Muhimu ili kujikomboa na mkoloni
mweusi.
Tunawaomba wanahabari watusaidie kuandika kwa kina mapungufu yaliyomo
kwenye Katiba pendekezwa. Ikiwezekana anzeni kutuandikia vipeperushi
kutuelezea mapungufu ya ibara kwa ibara. Wanaharakati jitokezeni
kumuunga mkono mzzee Joseph Waryoba, Mwalimu Nyerere Foundation
kutuelimisha kwa kasi.
Hizo Katiba pendekezwa tutazisikia kwenye radio tu maana hazijagawanywa
kwa wananchi. Sasa kama hawajampelekea Mzee Waryoba wewe na mimi
tutaipata kweli?
|
|
|
|
|
|
|
|
Hakuna maoni
Chapisha Maoni