Zinazobamba

CCM yakionya ACT kutochochea fujo Zbar

Na Mwandishi Maalum Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi (CCM )kimekitaka ACT  Wazalendo  kuacha kueneza upotoshaji na kudai kuwa  Uandikishaji wapiga kura  Mikoa wa Kaskazini " A" na 'B'  kuna baadhi ya wananchi hawakuandikishwa. 

CCM kimekanusha na kusema  wananchi wote  waliokidhi vigezo kwa vya sheria ya Ukaazi  na majina yao yamo kwenye Daftari la Sheha wa shehia, wote ameandikishwa.

Indhari  hiyo imetolewa na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar,   Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Mbeto  Khamis  Mbeto , akimkanya Naibu Katibu Mkuu ACT  Wazalendo  Zanzibar,  Omar Ali  Shehe .

Mbeto alimtaka Shehe aache kutoa  madai ya kutengeneza kinyume na ukweli dhidi ya watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC ), Kamati za Ulinzi na Usalama Mikoa , Wilaya  na Makatibu Tawala  SMZ kila wanapotimiza majukumu  yao ya kazi  .

'Shehe   kila wakati  amekuwa kiongozi   kichefuchefu anayekusudia  kuvuruga  taaswira ya utulivu   katika uandikishaji wapiga kura. SMZ ina  Vyombo vyake vya kiserikali  kuanzia Shehia hadi Serikali Kuu" Alisema Mbeto 

Alisema kwa kiongozi  anayejua mgawanyo  wa madaraka wa serikali ,  hawezi kumzuia  Mkuu wa Mkoa , Wilaya, Polisi , Maafisa wa Usalama au  Makatibu  Tawala wilaya na Mikoa,wasitimize wajibu wa  kazi zao . 

Mbeto  alisema Omar    Shehe  yaonyesha hatambui  hadhi ya  vyombo  hivyo na pengine haujui hata muundo wa Serikali , hivyo amekuwa akilipuka na kutoa shutuma,  akieneza uzushi na kufanya upotoshaji  wakati  zoezi  la Uandikishaji  likiendelea vizuri.

"Kinachofanywa na Omar Shehe ni utekelezaji wa  mpango  mkakati wao   batili  kuelekea  Uandikishaji  Wilaya  na Mikoa  mingine ya  Unguja . Anatamani uzuke  mtafaruku. Wanaochochea na walioandaliwa kufanya fujo watajulikanav"  Alieleza 

Mbeto katika maelezo yake  alisema ACT  wanajiandaa kuvunja sheria kwa kujaribu  kutaka kuwazuia watanzania waliotimiza vigezo  vya kisheria baada ya kukaa Zanzibar  miaka kumi mfululizo jambo  ambalo si sahihi  kwa mujibu wa sheria.

"Sheria  Namba 4 ya Mwaka 2018 imetaja   mzanzibari aliyeishi kwenye jimbo na  shehia  miezi thelathini na sita  mfululizo ataandikishwa kuwa mpiga kura. Kwa Mtanzania anayetoka Aisha  Mara ,Njombe, Sumbawanga au Mbeya aliyeishi  zanzibar miaka kumi  mfululizo nae  haki ya kuansikishwa na kupiga kura  " Alieleza Mbeto  

Mwenezi  huyo CCM, alisema mara kadhaa , amekuwa akimsihi  sana  Shehe  aepuke kutoa matamshi hatarishi badala yake  aonyeshe   ukomavu wake  kisiasa  lakini amekuwa akijifanya haambiliki na  hamnazo.

"Zoezi la Undikishaji linaendelea vizuri .CCM  imeshakusanya ushahidi wa matamshi ya vitisho yaliotamkwa na   viongozi wa ACT   kwenye mikutano ya hadhara .Tumevijulisha vyombo vya dola vipime matamshi  hayo na kuchukua  hatua mapema  " Alieleza Mbeto

Hakuna maoni