Zinazobamba

SPIKA NDUGAI AMFANYIA UKATILI FREEMAN MBOWE,AMPORA GARI ANALOTEMBELEA,SOMA HAPO KUJUA

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Bunge la Tanzania limeamuru kurudishwa nchini gari linalosaidia kumhudumia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) aliyelazwa nchini Kenya akipatiwa matibabu ya majeraha ya risasi aliyoyapata aliposhambuliwa na watu wasiojulikana mjini Dodoma Sptemba 7 mwaka huu, anaandika Mwandishi Wetu.
Gari hilo linatumiwa na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye yupo jijini Nairobi nchini Kenya akimuuguza Lissu tangu alipofikishwa hospitalini hapo akiwa mahututi.
Mbowe anatumia gari hilo kama haki yake kwa mujibu taratibu zilizowekwa ambazo zinasema kiongozi wa kambi ya upinzani anatakiwa kupatiwa usafiri pamoja na dereva.
Lakini Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini Kenya, dereva wa gari leo la serikali aliamuliwa kulirudisha nyumbani na kumuacha bosi ambaye ni Mbowe bila usafiri.
Imedaiwa kuwa gari hilo ambalo analitumia Mbowe lilikuwa linasaidia kazi ndogo ndogo zinazohusiana na kumhudumia Lissu lakini leo dereva ametakiwa kulirudisha nchini haraka.
Tangu Lissu apigwe risasi kumekuwapo na mizengwe mingi iliyolenga kukwamisha matibabu yake ikiwamo Bunge kukataa kumgharamia matibabu, kuchelewesha Sh. milioni 41 zilizochangwa na wabunge kwa ajili ya kumsaidia Lissu.


Kauli nyingine iliyozua utata ni pale serikali iliposema tangu ya kwanza kwamba Lissu kama anataka agharamiwe matibabu ni lazima aende kutibiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na siyo vinginevyo.