GAZETI HILI NALO KUFUATA NYAYO ZA MWANAHALISI,SERIKALI YAJIPANGA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU,SOMA HAPO KUJUA
Gazeti la Tolea la Raia mwema la jana ambalo limeibua mjadala mzito , |
GAZETI la Raia Mwema ambalo linatoka mara moja kwa wiki liko mbioni kufungiwa ama kupewa onyo kali na serikali ya Rais John Magufuli kutokana na kuandika kichwa cha habari kinachoelezwa kumchafua Rais.(Mtandao huu umedokezwa).Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Gazeti la Raia Mwema ambalo linatoka kila jumatano na ni miongoni mwa Gazeti ambalo linaandika habari za uchunguzi zenye Makala mbali za kisiasa na za kijamii.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa wa Fullhabari.blog kutoka ndani ya habari maelezo ambaye amekataa kutaja jina lake kutajwa mtandaoni amesema tolea la Gazeti la Raia Mwema t la jana tarehe 27 hadi tarehe 2 ya mwezi wa kumi mwaka huu lilikuwa na habari yenye kichwa cha habari “URAIS UTAMSHINDA MAGAFULI’ ambapo kichwa cha habari hichi kinatajwa kumkashifu rais.
“Ujue bwana hawa watu habari ya jana imetushtua sana,wahariri wa gazeti hilo wameitwa hapa waje kujitetetea kutokana na habari ile,maana habari hii inamkashifu rais hawezi ukasema Urais utamshinda"
"wakati nchi ipo vizuri amani ipo mambo
yanaenda kwahiyo hawa watu wamemkashifu rais kwahiyo wewe ngojea lolote kutoka serikali itakaloamua ”amesema mtoa taarifa wetu.
Taarifa hii
inakuja ikiwa ni wiki moja kupita baada ya serikali kulifungia kwa miaka miwili gazeti ambalo linatoka mara
moja kwa wiki la mwanahalisi kutokana na
kuandika habari ambazo zizotajwa kuwa ni za uchochezi.
Mbali na
Gazeti hilo kwa kipindi cha Miaka miwili tangie Rais Magufuli aingie madarakani
ni teyari serikali imeyafungia magazeti Zaidi
ya 400 kutokana na magazeti hayo kutochapishwa kwa mda mrefu huku baadhi yao
yakifungiwa kutokana kuandika habari zinadaiwa kuwa ni za uchochezi.
Fullhabari.blog
ilimtafuta Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo ,Dk Hassan Abbas lakini jitihada za kumpata hakikuzaa matunda kutokana na simu yake kutopatikana ili aweze kuzungumzia suala hili