Zinazobamba

MBUNGE MNYIKA AANZA MAKOMBORA KWA RAIS MAGUFULI,AMSHIKA PABAYA,SOMA HAPO KUJUA



John Mnyika, Mbunge wa Kibamba
Mbunge wa Kibamba John Mnyika



JOHN Mnyika, Mbunge wa Kibamba jijini Dar es Salaam ameanza kumchokonoa Rais John Magufuli kwamba, ahuishe Mchakato wa Katiba Mpya na kurejesha maoni ya wananchi, anaandika Regina Mkonde.

Amesema, hakuna sababu ya kubeba maoni yaliyotolewa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuyafanyia kazi badala ya yale ya wananchi yaliyokusanywa na Jaji Mstaafu, Joseph Warioba, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba.

Akizungumza na mtandao huu leo, Mnyika amesema kuwa, Rais Magufuli anapaswa kujua kwamba, ni jambo la msingi na busara kuheshimu maoni ya wananchi kwa kuwa wao ndio wanaopaswa kuamua hatma ya taifa lao.

Kauli hipo pia aliitoa siku mbili zilizopita wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wanasheria -Justice Voices Tanzania (JVT) unaoshirikiana na Shirika la Maendeleo la Kimataifa (UDI).
Kwenye uzinduzi huo Mnyika amemtaka Rais Magufuli na Harrison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria kutangaza siku ambayo Mchakato wa Katiba Mpya utaanza na kwamba, irejeshe rasimu ya Jaji Warioba.
Akizungumzia uzinduzi wa JVT Mnyika ambaye ni mlezi wa umoja huo ameitaka serikali kuweka kipengele cha huduma za kisheria katika Katiba kutokana na kwamba, huduma hiyo ni haki ya kila Mtanzania.
“Wananchi wote wana haki kisheria ya kupata huduma za kisheria ambazo kwa sasa huzikosa kwa sababu ya kutokuwa na uwezo wa kugharamia,” amesema Mnyika.
Edward Kinabo ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa UDI amesema, siku ya uzinduzi wa JVT walihudumia watu 23 na kwamba, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika hilo, siku chache zijazo wanatarajia kuhudumia maelfu ya watu.
“Tunajipanga kutanua wigo wa huduma hizi ili zifike hadi mikoani, licha ya hivyo siku ya uzinduzi ilitakiwa tuhudumie watu wengi zaidi lakini tulikwama kufika kutokana na mvua,” amesema.
Judith Kapinga, Mwanzilishi kiongozi wa JVT anasema lengo la kuuanzisha umoja huo ni kutoa msaada wa huduma za kisherai kwa wananchi wasio na uwezo wa kuipata huduma hiyo ili kuwaepukana na umasikini unaosababishwa na ukosefu wa haki.
“Lengo letu ni kutao msaadakwa wananchi wa kipato cha chini kwa kuwa tunaamini kwamba umasikini hautokani na ufisadi tu bali ukiukwaji wa haki za binadamu nachangia kurudisha nyuma maendeleo ya watu,” amesema Kapinga.
Kapinga anafafanua mifano ya ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwa pamoja na matukio ya kubomolewa makazi, migogoro ya ardhi na kudhurumiwa mirathi.
J.V.T na U.D.I kwa sasa inatoa huduma kwa wananchi waishio katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, na kwamba hapo baadae wanatarajia kutoa huduma hiyo nchini kote.

Hakuna maoni