Zinazobamba

MANJI AKWAMA TENA MAHAKAMANI,SOMA HAPO KUJUA

KESI ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji, imeahirishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo.

Akiieleza mahakama hiyo, wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena.

Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na plate number mbili za magari ya serikali.

Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.