JUKWAA LA KATIBA: HATUKUBALIANI NA UTAJAJI MAJINA USIO NA TIJA,..
Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) limeibuka na kupinga tabia ya kutaja majina ya watu wanaodaiwa kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya pasipo kufuata taratibu za Nchi, wakisema kufanya hivyo kunaweza kuleta athari kubwa kwa watanzania ikiwamo kulipa fidia nyingi kama ikibainika kuwa waliotajwa hawahusiki na biashara hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa habari, ofisini kwake Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bw. Deus Kibamba amesem Jukwaa hilo linaamini katika utawala wa sheria, na kushauri kuwa ni busara kwa vinara wa vita hii kufanya uchunguzi kabla ya kuwataja hadharani na kuchafua maisha ya watu.
"Utajaji wa majina una athari mbili moja ni kulipa fidia kama ikibainika waliotajwa hawahusiki, lakini la pili ni muendelezo wa chuki kati ya kizazi na kizazi kutokana na majina hayo. ni heri zoezi hilo likafanywa na watu wenye weledi ambao wamesomea taaluma ya uchunguzi."
Aidha akizungumzia
Juu ya kukwama kwa mchakato wa katiba mpya nchini na Jinsi ya kuuanzisha Upya
Deus amesema JUKATA wamejipanga kuhakikisha kuwa mchakato huo unahishwa ili taifa lipate katiba mpya.
Katika hatua nyingine
JUKATA pamoja na kulaani watu wanaotumia lugha za matusi kuwakosoa viongozi
wakuu wa nchi lakini hatua ya kuwakamata na kuwaweka ndani watu kwa makosa ya
kukosoa kwa lugha nzuri bila matusi ni kinyume cha katiba ya Tanzania huku
wakisisitiza kuwa hakuna kiongozi bora duniani asiyekubali kusikia mawazo ya
kukosolewa kutoka kwa wananchi wake.
Kibamba amesema kuwa
uvumilivu wa kisiasa unahitajika sana katika nchi kipindi hichi ambacho nchi inaongozwa na serikali mpya kwa
kuwa kumekuwa na matukio ambayo yanatisha ikiwemo watu kupotea bila kujulikana
walipo,na wengine kukutwa wakiwa wamefariki katika viroba na serikali kushindwa
kutoa maelezo yaliyokamilika kuhusu matukio hayo.
Aidha katika hatua
nyingine Mwenyekiti huyo wa JUKATA amesema kuwa kulingana na matukio mbalimbali
yanayoendelea kutokea nchini sasa ni wazi kuwa nchi inahitaji katiba mpya sasa
na sio siku nyingine hivyo wao kama JUKATA wameanza Rasmi mchakato wa kufufua
harakati za kupata katiba mpya nchini.
Moja kati ya mambo
ambayo ameyataja kuwa wameanza nayo katika kufufua mchakato huo ni pamoja na
kufanya mkutano mkuu wa katiba ambao utafanyika kuanzia Tarehe 2 hadi 3 mwezi
wa Tatu ambao utawashirikisha wadau mbalimbali wa katika nchini, pamoja na uzinduzi
wa Filamu mpya ya Dakika 20 itakayokuwa inaonyesha mchakato mzima wa katiba
mpya.
Katika hatua nyingine
JUKATA wametuma wito wa kufanya mazungumzo na Rais Wa Jamhuri Ya muungano wa Tanzania
Mh Dr John Pombe Magufuli kwa ajili ya kujadili naye maswala mbalimbali
yanayohusu Katiba mpya nchini pamoja na kumshauri Mambo kadhaa ya kupata katiba
Mpya.