Zinazobamba

DC HAPI AWASIHI WATENDAJI KINONDONI,NI KUHUSU FEDHA ZA MIRADI,SOMA HAPO KUJUA


Pichani aliyevaa suti ni MKuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi akisikiliza kero kutoka kwa wananchi wakati alipokuwa kwenye ziara zake kwenye kata 10 ndani ya Manispaa hiyo kwa lengo la kukagua mipango ya maendeleo pamoja na kuwasikiliza kero wananchi

NA KAROLI VINSENT
Mkuu wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi amewataka  watendaji wa kata kuzisimamia fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya miradi maendeleo ili kuweza kuziokoa fedha hizo kupotea.

Pia,Hapi amewaagiza watendaji hao kuhakikisha fedha inayotenga kwenye mradi husika ilingane na thamani harisi ya fedha.

Mkuu huyo Wilaya ,ameyasema hayo leo Wakati alipokuwa kwenye ziara katika Kata ya Bunju ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya Siku 10 ,ziara hiyo yenye lengo la kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Amesema nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha fedha za serikali hazipotei hivyo anawahimiza watendaji wa serikali za mitaa kuhakikisha wanasimamia fedha zilizotengwa kwenye miradi.

"Hizi milioni 700 mlizopewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo hakikisheni mnazitumia kwa uangalifu na umakini ili zisipotee hovyo,hata hiyo miradi ya maendeleo inayojengwa ilingane na thamani ya fedha"amesema Hapi.

Amesema kuna baadhi miradi inayotekelezwa hailingani na thamani ya fedha iliyotengwa jambo analozidi wahimiza kusimamia kwa umakini fedha.

Hata hivyo,Hapi amewata watendaji wa kata kuhakikisha wanayaweka maeneo hayo kwenye mipango (master Planning) ili kuweza kuyabaini maneo ya wazi katika eneo husika.

"Ninavyoka kila kata kuwa master Planning lengo ni kutaka kujua maeneo yapi ya wazi yalivamiwa ,maana kwa sasa Kinondoni,hatutaki kuwa kama wenzetu huku nyuma ambao waliruhusu maeneo ya wazi kuvamiwa,nataka niwahakikisha kwa sasa sisi tutakuwa wakali sana kwenye maeneo ya wazi yaliyochukuliwa na watu ili yaweze kurudi,”amesema Hapi.