Zinazobamba

RAIS MAGUFULI AANZA KUGONGA "MWAMBA",AHADI YA MIKOPO KWA WANAFUNZI YAANZA KUFIFIA,SOMA HAPO KUJUA



 
RAIS John Magufuli amekiri ‘kugonga mwamba’ kwa ahadi ya serikali yake kwamba, hakuna mwanafunzi wa Chuo Kikuu atakayecheleweshewa mkopo na kama ikitokea hivyo, mtumishi wa serikali aliyehusika na suala hilo atapoteza kazi, anaandika Pendo Omary.

Magufuli alikuwa akizungumza katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alipoenda kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa majengo 20 ya mabweni ambayo yatakuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 3,846.
Rais Magufuli, Oktoba mwaka jana alipokuwa akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Jimbo la Tabora Mjini mkoani Tabora alisema; “Huwezi kumtoa mwanafunzi Kaliua (Tabora), kwenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, awe amefaulu kwa daraja la kwanza au la pili halafu afike pale chuoni fedha zake hujamuingizia wakati bodi imeshamteua kwenda masomoni.

Kama umemteua kwenda Chuo Kikuu, hukujua kuwa anatakiwa kupata mkopo? Serikali ya Magufuli, ukimcheleweshea mkopo mwanafunzi ujue kazi huna,” alisema na kushangiliwa.
Rais Magufuli katika hotuba yake aliyoitoa leo UDSM ameishia kulalamika kuwa mawasiliano mabovu kati ya Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu (HESLB) na Wizara ya Elimu ndiyo yamesababisha wanafunzi kutopewa fedha za mikopo mpaka sasa.
“Hakukuwa na Coordination (uratibu), tangu mwanzo ilitakiwa vyuo vikuu vyote ya Elimu ya juu viwe na tarehe moja ya kufungua. Unafungua chuo haraka halafu unataka wanafunzi wafanye usajili wakati bodi ya mikopo haijalipa,” amesema Magufuli.
Kinyume na ahadi yake kwamba ucheleweshaji wa mikopo ukitokea, atawafukuza kazi watumishi waliohusika, leo Rais Magufuli ‘amegwaya’ kutangaza kumchukulia hatua mtumishi yoyote aliyehusika na uzembe huo wala kueleza hatua zozote atakazochukua kutokana na ucheleweshaji huo wa mikopo.
Itakumbukwa kuwa, mpaka sasa ni wiki mbili tangu wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa UDSM, waanze kuripoti chuoni hapo lakini serikali imeshindwa kuidhinisha malipo ya fedha zao za kujikimu huku wanafunzi hao pia wakigomea kusaini fedha ya kujikimu iliyo pungufu, tofauti na utaratibu.
Pia ni siku sita sasa tangu wanafunzi wa mwaka wa Pili, Tatu na mwaka wa Nne waanze kuripoti chuoni hapo lakini serikali imeshindwa kuwapatia fedha zao za kujikimu, jambo linalowapa wakati mgumu kujikimu kwa chakula na malazi.
Rais Magufuli amesema tayari Wizara ya Fedha imetoa Sh. 80 bilioni za awali kwa ajili ya kulipia mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu huku akisema serikali haitatoa fedha kwa wasiostahili kupata mikopo