Zinazobamba

NIA YA TAMWA KUHUSU MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAHABARI


 
Chama cha Wanahabari wanawake Tanzania -TAMWA kimeamua kuungana na Watanzania, Serikali na wadau wote katika kupambana na ajali za barabarani zinazoweza kuzuilika, ili kuokoa vifo vya watanzania baada kuanza utekelezaji wa mradi wa usalama barabarani.
 
 Mradi wa usalama barabarani una lengo kubwa la kuona  kwamba, wanahabari wanapata weledi wa kuandika habari hizi kwa mapana yake, lakini hasa kwa kuzingatia kuwa wanatoa elimu kwa jamii ya Tanzania kuhusu masuala ya usalama barabarani.
 
 Kwa kuanza TAMWA imeendesha mafunzo ya siku tatu kwa wanahabari ili kuwajengea uwezo wa namna ya kuandaa habari hizi.
 
 Awamu ya pili na tatu ya mafunzo itafuatia siku chache  zijazo. TAMWA inaamini kuwa wananchi wengi watapokea elimu hii kwa kusoma habari katika magazeti, na kusikiliza Radio na hata kuona vipindi mara kwa mara kutoka kwenye televisheni.
 
 Kutokana na idadi kubwa ya vifo vinavyosababishwa na ajali za barabarani, ambavyo hutokea kwa kiwango cha kutisha nchini.  
TAMWA inaona kuna umuhimu wa kuvalia njuga suala  hili kwa kushirikiana na wenzetu (wadau) kama vile wanasheria kwa kuzifanyia marekebisho sheria na kanuni za usalama barabarni ili kuipa nguvu 'Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 1973’, sheria ambayo kwa njia moja au nyingine itaweza  kudhibiti watumiaji wanaokiuka matumizi sahihi ya barabara. 
 
 Maeneo ambayo yanapaswa kuzingatiwa katika marekebisho ni; mwendo kasi, ulevi wakati wa uendeshaji, uvaaji kofia ngumu, kufunga mikanda na vizuizi kwa watoto.
 TAMWA inatambua kwamba wanawake wengi na watoto ndio wenye kubeba mzigo mkubwa unaotokana na ajali barabarani, ingawa takwimu zinaonyesha kuwa  waathirika wa juu wa usalama barabarani ni wanaume.
 
 Ila ukweli ni kwamba wanawake na watoto ndio wanaoathirika zaidi kwani watoto hukosa huduma na mahitaji  ya msingi baada ya kupoteza watu wanaowategemea