Zinazobamba

TAARIFA MUHIMU KUTOKA PPRA LEO,SOMA HAPO KUJUA



 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEivTPG8ROTsfd_FpM2pGB6ObGAXf5OOdH3xgUfl5xbwN0rSwSiZmQFmwBa1nU6uCFP-9uRcUSxFvOxXUaMVzZhnwfCPKTmUPT7Vx8_MKvAlnhW_rhE9xBw1iRGcwR3gDR6FO_JFIZlsiOQ/s1600/WhatsApp+Image+2016-09-30+at+5.33.09+PM.jpeg

RIPOTI ya Ukaguzi kwenye manunuzi ya umma ya mwaka wa fedha 2015/2016 uliofanywa na mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) unaonyesha taasisi  10  nunuzi  zimefanya  manunuzi chini ya kiwango kisichoridhisha chini ya asimia 60.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga amesema taasisi hizo zimefanya chini ya kiwango katika kufanya manunuzi  yake  kwa  mujibu wa sharia ya manunuzi.

Amesema jumla ya PPRA imefanya  jumla ya mikataba 21,313 ya manunuzi yenye thamani ya sh.Trioni 1.05 katika ujenzi ,vifaa, huduma ushauri wa kitaalam .huduma zilizohitaji mikatba ya ushauri wenye thamani ndogo  pamoja na mikataba yenye makubaliano maalum.


Balozi Lumbanga amezitaja taasisi zilizofanya chini ya kiwango ambazo ni Taasisi ya Uzalishajin (NIP), Dar es Salaam Rapid Transist (DART), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Makumbusho ya Taifa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), Taasisi ya Mifupa (MOI), Halmashauri ya Manispaa ya Msoma pamoja na Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Bukoba (Buwasa).

Amesema mikataba 122 ya ukusanyaji wa mapato iliyokaguliwa kwenye mamlaka tisa ya serikali za mitaa kwa mujibu wa mikataba iliyokaguliwa imebainika kuwa na mapungufu kadhaa katika usimamizi wa mikataba hiyo na kufanya halmashauri kushindwa kukusanya kiasi cha sh. Milioni 761.54.




Aidha Balozi Lumbanga amesema kuwa kushindwa kukusanya mapato hayo Halmashauri zimesababisha hasara halmashauri hizo zimeshindwa kuchukua hatua zozote dhidi ya wazabuni waliopewa miradi kutokana mikataba walioingia.