SERIKALI YAENDELEA NA SINEMA,NI KUHUSU WATUMISHI HEWA,YAJA NA HIKI TENA,SOMA HAPO KUJUA
Na Frank Shija, MAELEZO
SERIKALI inatarajia kufanya zoezi la utambuzi na
usajili wa taarifa za watumishi wa umma kuanzia tarehe 3 Oktoba ili kutoa
vitambulisho vya Taifa vilivyo na taarifa zote muhimu za mtumishi husika.
Hayo yamebainisha na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angellah Kairuki alipokutana na
waandishi wa habari ofisini kwake jana Jijini Dar es Salaam.
Kairuki alisema kuwa zoezi hilo la utambuzi na
usajili wa wananchi ambalo linaanza na watumishi wa umma ni muhimu na
litasaidia kupunguza gharama kwa Serikali na kuondoa usumbufu kwa wananchi
kwani taarifa zao zote muhimu zitakuwa sehemu moja hivyo kupunguza kero ya kuulizwa
taarifa kila uendapo.
Waziri Kairuki alisema kuwa zoezi hilo
litashirikisha Wizara yake pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), ambapo taarifa
zitakazotumika ni zilizilizopo katika vitambulisho vya mpiga kura.
“Kama mnavyofahamu kuwa Serikali ipo
katika maboresho makubwa ya utendaji wake, hivyo ili kuendana na hali hiyo
tutaanza zoezi la utambuzi na usajili wa watumishi wa umma kuanzia tarehe 3
Oktoba, zoezi litakalochukua takribani wiki mbili, zoezi hili ni muendelezo wa
Serikali kukabiliana na matatizo ya kutokuwa na taarifa sahihi.” Alisema
Kairuki.
Aidha Kairuki aliwata watumishi wote wa umma
kushiriki zaoezi hilo wakiwa na taarifa zote muhimu zinazowatambulisha ambazo
ni pamoja na Cheti cha kuzaliwa, vyeti vya elimu, kitambulisho cha kazi,
Kitambulisho cha Mzanzibar Mkazi, hati ya malipo ya Mshahara, hati ya kusafiria
na kadi ya mpiga kura.
Waziri huyo ametoa wito kwa waajiri kuweka mazingira
wezesha ili kufanikisha zoezi hilo ikiwemo kutenga ofisi itakayotumiwa na kwa
kazi hiyo pamoja na kusisitiza waajiri wahakikishe watumishi wao wanasajiliwa
bila kukusa na taarifa ya zoezi hilo iwasilishe Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawabora ndani ya siku 14 tangu zoezi hilo kukamilika
kwake.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Laurian Ndumbaro aliwataka
watumishi wote wa umma kulipa umuhimu mkubwa zaozi hilo na kusisitiza kuwa
Serikali haita sita kucghukua hatuia za kinidhamu kwa mujibu wa kanuni za
utumishi wa umma kwa mtumishi yeyote atakaye kaidi zoezi hilo.
Awali akijibu swali la mwandishi wa habari kuhusu
namna zoezi hilo litakavyotekelezwa nchi nzima kwa muda wa wiki mbili tu, Kaimu
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mohammed Khamis Abdallah
alisema kuwa zoezi hilo litafanikiwa kwani wanao wafanyakazi zaidi ya 460 nchini
nzima ambao wapo katika Ofisi za Halmashauri.
Pia aligusia suala la vifaa na kusema kuwa tayari
wamewasiliana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo imewapa mashine za BVR kwa
ajili ya kuzitumia katika zoezi hilo la utambuzi na usajili.
Zoezi la utambuzi na usajili wa wananchi hasa
watumishi wa uuma kukabiliana na vyanzo vya watumishi hewa kwa kuunganisha
mifumo ya utambuzi wa watu na mifumo mingine ikiwemo usimamizi wa rasilimali
watu na mishahara katika utumishi wa umma ambapo kuunganishwa kwa mifumo hiyo
kutawezesha mifumo hiyo kuwasiliana na kutumia taarifa zilizo kwenye kanzi data
ya NIDA suala litakalokuwa limerahisisha upatikanaji wa taarifa