MOROGORO KUANDAA KONGAMANO LA UWEKEZAJI KUTANGAZA FURSA ZILIZOPO MKOANI HUMO,SOMA HAPO KUJUA
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven
Kebwe akizungumza na waandishi wa habari katika Mkutano uliofanyika kwenye
Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Jijini Dar es salaam juu ya uwepo wa
Kongamano la Uwekezaji litakalofanyika Mkoani Morogoro Septemba 29-10, 2016
lenye lengo la kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Mkoani humo,
kwani umejaaliwa kuwa na mazingira mazuni na uwepo wa rasilimali nyingi ambazo
bado hazitumika ipasavyo, pia amewataka vijana wa kitanzania kuacha
kukimbilia mijini na badala yake wajikite kwenye fursa ya uwekezaji wa kilimo
na ufugaji. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini
(TIC), Clifford Tandari.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Clifford Tandari akifafanua jambo katika Mkutano huo na Waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es salaam juu ya uwepo wa Kongamano la Uwekezaji Mkoani Morogoro litakalofanyika Septemba 29-10, 2016 , ambapo amesema kuwa Kongamano hilo litasaidia kuutangaza Mkoa wa Morogoro kama miongoni mwa maeneo yenye fursa na mazingira mazuri ya kibiashara kwa Makampuni ya ndani na nje ya nchi.
Mkutano huo ukiendelea.