Zinazobamba

WANAHARAKATI WA HAKI ZA BINADAMU WAMUONYA JPM,NI KUHUSU OPARESHENI UKUTA YA CHADEMA,SOMA HAPO KUJUA




Kituo cha Sheria na Msaada wa Haki za Binadamu (LHRC) kimemshauri Rais John Pombe Magufuli kufuta kauli zenye utata kwa madai kuwa zinakiuka haki za binadamu na siasa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari, leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk. Helen Kijo Bisimba amesema kauli hizo zinaweza zikaathiri mtu mmoja na jamii kwa ujumla endapo zikiwa kinyume na sheria pamoja na katiba za nchi, “Kituo kinatambua nguvu ya kauli ya Rais Kuwa hutoa agizo la kiutekelezaji wa vyombo vyote serikalini na ikiwa kinyume inaweza ikasababisha madhara makubwa kwa mtu mmoja ama jamii kiujumla, ”Alisema Bisimba


Bisimba amemsisitiza Rais Magufuli kufuta kauli zenye utata ikiwemo kauli ya kufuta shughuli za kisiasa mpaka mwaka 2020 kwa kuwa iko kinyume na Ibara za 3(1) na 20(1) ya katiba na vyama vya siasa, “Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia haki za siasa zikikandamizwa kwa matamko ya viongozi mbalimbali wa juu wa serikali akiwemo Rais Magufuli mfano akiwa ziarani mkoani singida alitoa tamko la kuzuia shughuli zote za kisiasa hadi mwaka 2020,” amesema na kuongeza.
“Pia Waziri mkuu Kassim Majaliwa akiwa Ruangwa Lindi alitoa tamko la kuzuiwa mikusanyiko yenye mlengo wa kisiasa ingawa alikanusha tamko hilo alipokuwa bungeni, wakuu wa mikoa pia walitoa matamko mbalimbali la polisi kuzuia sehemu nyingine wanasiasa wasikutane”
Amesema kutokana na kauli hizo imeshuhudiwa baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa kutoa matamko na maazimio yenye kuashiria chuki, uhasama na sintofahamu kwa jamii na kuelekea kuuvunja umoja na amani ya Taifa, “Msajili wa vyama vya siasa asimame katika nafasi yake ya mratibu, msimamizi na mbeba bendera ya maendeleo ya vyama vya siasa na ukuaji wa demokrasia na kutojiingiza katika kuonekana kuegemea upande au chama chochote, ili kusaidia kujenga mshikamano wa Taifa.