Zinazobamba

MIAKA 40 YA TAZARA,WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI DAR WAJIFUNZA MENGI LEO KUHUSU TAZARA


Wanafunzi wa shule za msingi mbalimbali mkoani Dar es salaam wakishangilia kwa furaha wakati wa ziara ya wanafunzi hao waliyoifanya katika mamlaka ya reli Tanzania na Zambia TAZARA ambapo ziara hiyo ni moja ya shamra shamra za kuadhimisha miaka 40 tangu kuanza kwa mamlaka hiyo.Akizungumza na ,mtandao huu afisha Uhusiano wa Tazara kwa Upande wa Tanzania Bi Regina Tarimo amesema kuwa wanafunzi zaidi ya mia Tano wamepata nafasi ya kutembelea Mmlaka hiyo na kujionea utendaji kazi wa Reli za Tazara ambapo pia walipata nafasi ya kupanda Treni moja wapo kutoka Makao makuu ya Tazara hadi Kituo cha MWAKANGA na kurejea ikiwa ni moja ya Tukio la kuwafanya wanafunzi kuelewa kwa undani Jinsi TAZARA inafanya kazi zake hapa nchini
Afisa uhusiano wa TAZARA kwa upande wa Tanzania REGINA TARIMO akiwaeleza maswala mbalimbali pamoja na kujibu maswali ya wanafunzi hao walipotembelea Katika maonyesho ya TAZARA ambayo yanafanyika kuonyesha maswala mbalimbali yanayofanyika TAZARA ikiwa ni maadhimisho ya miaka 40 yake,
Furaha ya kupanda Treni Ya TAZARA na kujionea shughuli za Mmlaka hiyo zilitawala Nyuso za wanafunzi hao leo

 
Walimu nao wakipata maelekezo kwa kina Kuhusu TAZARA(Picha zote na Habari24)