Zinazobamba

HATIMAYE VIONGOZI WA DINI WAOKOA JAHAZI HILI LA WAPINZANI,SASA WAFANIKIWA KUMALIZA MTEGO HUU,SOMA HAPO KUJUA



 

NA KAROLI VINSENT
HATIMAYE viongozi wa dini nchini wameweza kutatua mtego wa kwanza wa vyama vya Upinzani nchini,baada wa  vyama hivyo  kukubali kurejea kwenye Bunge la Jamhuri wa Muungano na kushiriki vikao vyake. vinavyotarajia kuanza hivi karibuni

Awali Wabunge wa upinzani walikataa kushirika vikao vyote vya bunge hilo ambavyo vitaongozwa na Naibu Spika DK Tulia Acksoni kwa madai kuwa kiongozi huyo anaendesha bunge hilo kibabe.

James Mbatia ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi  akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Vyama vinne vyenye wa Wabunge kwenye Bunge hilo, ambavyo  ni  Chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema),Chama cha Wananchi (CUF)  na chama cha Act Wazalendo.


Amesema wamefikia hatua ya kukubali kurejea bungeni kutokana kukubali ombi la viongozi wa dini waliokutana nao kwenye kikao cha siku mbili  walichokaa jana na  juzi ambapo katika kikao hicho Kilihudhiriwa na viongozi mbali mbali wa dini ambapo kiliitishwa na viongozi hao kutaka suluhu ya mtafaruku wa kisiasa unaendeleo nchini ili kulinusuru taifa na mchafuku yanaweza kutokea. 

Amesema nia ya vyama hivyo si kuleta  fujo bali na kuijenga amani ya Tanzania, amedai kuwa wamewaeleza Viongozi hao wa kidini sababu ya wao kutoka bungeni imetokana na Naibu spika kutokuwa mzelendo  kwa hatua yake ya kutoweka maslahi ya taifa huku akiendelea kukitetea chama chake.
Hata hivyo,Mbatia amesema baada ya wabunge hao kukubali kurejea bungeni  hatua inayofuta ni ya wao kututana na wabunge wote wa Upinzani na kuwaeleza ombi lao hilo na kulitekeleza.

Kwa Upande wake Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo,Ado Shaibu amemtaka Rais John Magufuli kupeleka mswaada Bungeni ambao ni wa   kuvifuta vyama vya Upinzani ili abaki yeye awe anaongoza nchini.
Amesema hatua yake ya kuvikandamiza vyama vya upinzani hakikubaliki huku akidai kuwa wao ACT-Wazalendo watapambana mpaka kuhakikisha haki yao ya msingi inaheshimiwa ya kufanya siasa nchini.
Ameeleza kuwa kwa sasa wanangojea barua kutoka Chadema ili nao waweze kujiiunga na Oparesheni ya Kupinga Udiktea nchini (UKUTA).
  KUHUSU MAANDAMANO NA MIKITANO YA HADHARA TAREHE 1 SEPTEMBA.
Mbatia ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Vunju,amesema kwa sasa wanaendelea na vikao usiku na mchana kuangalia kama kutapatikana suluhu kwenye suala hilo.
Amesema kwa sasa viongozi wa dini waliokutana nao baada ya kuzungumza nao walipanga kukutana na Rais Magufuli huku wakiwahidi wakitoka huku watakuja kuongea na Viongozi wa Upinzani.
Sanjari na hayo,Mbatia amelitadharisha jeshi la Polisi nchini kuacha kutumika kisiasa kwa kuingiza mambo ya jeshi hilo na siasa,
Amesema hatua ya jeshi hilo kuyahusisha mauaji ya Polisi wa nne wa jeshi hilo lilotokea Mbagala Jijini hapa na kulisusisha na harakati za siasa nchini ni kuliahabisha jeshi hilo na kuchangia kuleta hofu kwa jamii.
Amedai kuwa hata katazo walilotoa kwa vyama vya siasa kutofanya mikutano ya ndani kunazidi lionyesha jeshi hilo kufanya kazi kichama zaidi.